Friday 22 May 2015

MFAHAMU SR. IRENE STEFAN a.k.a NYAATHA - MWENYEHERI WA KWANZA KUTANGAZWA NCHINI KENYA

Wakati nchi ya Kenya inajiandaa na shmra shara za kutangazwa Mwenyeheri kwa Sr. Irene Stefani, Tanzania na nchi zingine za Afrika ya Mashariki yapasa pia tuone fahari hiyo. Wakati wa Vita ya kwanza ya dunia alihudumia wapiganaji walioumia vitani na inasemekana wengine walikuwa nai askari wa Kitanzania.
Sr. Irene Stefani


LAKINI, SR. IRENE STEFANI AU NYAATHA NI NANI HASA?



Sr. Irene, mama wa huruma na upendo alizaliwa nchini Italia Tarehe 22, Agosti mwaka 1891 na alifariki nchini Kenya, Octoba 31 ya mwaka 1930.Mama wa mapendo na huruma ni sentensi inayojumuisha maisha ya Sr. Irene, maisha ya kujitoa kwa Mungu  kwa ukarimu katika huduma na uinjilishaji.
Mwaka 1911, akiwa na umri wa miaka 20, Irene aliamua kuwa mmisionari wa shirika la Consolata, lililokuwa limeanzishwa huko Turin Italia na Mwenyeheri Joseph Allamano mwaka mmoja nyuma. Januari 29, mwaka 1914,  Sr. Irene aliweka nadhiri zake huko Turin alielezea programu yake ya maisha katika sentesi fupi akisema;
    "Ni Yesu pekee, Kabisa na Yesu, kuwa mali ya Yesu kabisa, Kabisa kwa ajili ya Yesu, fanya haya na utaishi"
Sista Irene alifika Kenya Januari 1915 na huko aliishi maisha ya waanzilishi wa kwanza, yaani; katika umaskini mkubwa, kazi ngumu na  kutengwa.
Moyo wake wa ukarimu haukujua mipaka ya kujitoa mwenyewe kwa mapendo makubwa na huruma akiwatangazia wote lulu zake kubwa amnao ni Habari njema kwamba Yesu, mwana wa Mungu, alikuwa ni mkombozi wao.

Mama wa Upendo na Huruma  




Miezi michache baada ya kufika Kenya, Vita vya kwanza vya dunia ndio vilikuwa vimefika katika makoloni ya Kijerumani na ya Kiingereza huko Afrika ya Mashariki.
Sr. Irene aliomba kujitolea katika shirika la Msalaba mwekundu ambao walikuwa wamejikita katika kazi ngumu za huruma kama vile, kuwahudumia waliumia katika hospitali za jeshi ambazo zilikuwa zimefurika wagonjwa wengi hasa wale walioumia.
Kwa muda wa miaka mitatu, Sr. Irene alijitoa kishujaa kuwahudumia kwa upendo na huruma watu waliolazimishwa kwenda vitani na kutelekezwa kufa baada ya kuumia.
Baada ya vita, Sr. Irene alirudi kwa wapendwa wake wakikuyu ambao walikuwa wamejizamisha katika kazi ya uinjilishaji, unesi, ualimu a kutembelea familia kila mara wakiwa tayari kusaidia, kutia moyo, kuongoza kwa upole vijana ili waweze kuishi imani yao ipasavyo. Kila mahali alifanya kazi kikarimu mno hadi watu wakamuita "Nyaatha" maana yake "Mama mwenye huruma"
Mwaka 1930 ulikuwa mgumu katika shirika lao jipya na kwenye Missioni. Sr. Irene aliyatambua haya yote hivyo aliwaomba wakuu wake aweze kujitolea maisha yake maskini kwaajili ya Misheni. " Siwezi kusema hapana - alisema mama Mkuu wa Shirika, mama Ferdinanda, lakini wacha tuyafanye mapenzi ya Mungu, hakuna zaidi ya kufanya mapenzi ya Mungu"

Sr. Irene alikuwa amepewa ruhusa kubwa ila hakujua kwamba Mungu angejibu haraka namna ile na kumchukua. yaani, wiki mbili tu baadae, Sr. Irene aliaga dunia/ alifariki. Alikufa kutokana na ushujaa wake wa upendo, kwa ugonjwa wa mlipuko uliotokea katika kijiji kimoja naye akaenda kuhudumia.

Hii ilikuwa ni Octoba ya mwaka 1930.



Masalia ya mwili wa Sr. Irene




Juu na chini ya vilima vya Kikuyu, habari zilipokelewa kwa maombolezo makubwa ambayo hayakuwahi kutokea kwamba Nyaatha- mama wa upendo na huruma, alikuwa amewatoka. Mabaki ya mwili wake sasa yapo katika Kanisa la Consolata, Nyeri huko Kenya. Hata baada ya miaka 50 ya kifo chake,  kumbukumbu zake bado zingali zinaishi katika mioyo ya watu.
Hata leo, Bado Sr. Irene Nyeri anaendeleza umisionari wake wa upendo na huruma.
Basi akiwa anatangazwa Mwenyeheri hapo Kesho, Sherehe zitakazoongozwa na Mwadhama John Kardinali Njue Askofu mkuu wa Nairobi na hati ya uenyeheri itasomwa na Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo Askofu mkuu wa Dar es Salaam -Tanzania, Wana Afrika ya Mashariki, yapaswa tuione sherehe yetu hii kama ni yetu sote na tumuombe maombezi yake ili amani itawale katika nchi zetu. 

Mwadhama Polycarp Kardinali. Pengo

Watu mbalimbali wakitembelea mahali amabapo Masalia ya Sr. Irene yamewekwa.
Mojawapo ya miujiza ambayo imefanikisha kutangazwa mwenye heri ni kipindi cha ukoloni kule Msumbiji ambapo makatekista na watu waliokimbilia kanisani kutengwa huko bila msaada wowote na hakukuwa hata na maji. Makatekista walisali kwa maombezi ya Sr. Irene basi maji ya liyowekwa kwaajili ya ubatizo yalijaa na watu waliyatumia kwa kunywa na kuoga kwa siku tatu.
Mwezi mmoja kabla ya kifo chake, Irene alienda kwenye mafungo ya Kiroho, huko alimsikia Bwana Yesu akimwambia " Dhambi zinanisulubu sana, yani ni heri maelfu wafe kuliko mtu mmoja kutenda dhambi"
Sr. Irene alipokaribia kufa wanawake walioenda kumuona walilia sana lakini yeye aliwaambia kwamba msilie mimi nakwenda mbinguni. Alikufa akiyataja majina ya Yesu, Maria na Yosefu.

Historia hii fupi ya Sr. Irene imetafsiriwa kutoka : http://www.irenestefani.altervista.org/inglese/biografia_en.html na http://mobile.nation.co.ke/news/Pope-puts-nun-who-worked-in-Nyeri-on-path-to-becoming-saint/-/1950946/2587262/-/format/xhtml/-/7kjtcq/-/index.html



Katika upendo wa Kristu,

Vincenzia- Marie!




No comments:

Post a Comment